• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Wajasiriamali wadogo wadogo kunufaika

Imechapishwa: June 11th, 2020

Mheshimiwa mkuu wa Wilaya ya Babati Bi. Elizabeth Kitundu akiambatana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati Ndg. Fortunatus Fwema, leo tarehe 11 Mei 2020 amezindua zoezi la ugawaji wa vitambulisho kwa wajasiriamali wadogo wadogo na wamachinga. Zoezi hilo liliambatana na ugawaji wa vitambulisho kwa baadhi ya wajasiriamali wadogo wadogo ikiwa ni ishara kwamba zoezi limezinduliwa rasmi. Akiongea na wananchi wa Mji wa Babati katika eneo la Machinga complex lililopo karibu na Soko kuu la Mji wa Babati, mheshimiwa mkuu wa wilaya amewaeleza wananchi juu ya umuhimu wa vitambulisho hivyo kwa wajasiriamali wadogo na wamachinga. 

Ugawaji wa Vitambulisho kwa baadhi ya wajasiriamali wadogo wadogo Mjini Babati


Nae afisa Biashara halmashauri ya mji Babati Bw. Chediel Fue ametoa ufafanuzi wa kina juu ya vitambulisho hivyo kwaajili ya wajasiriamali wadogo. Amewatoa hofu wajasiriamali wadogo wadogo na wamachinga wote kuwa wajisikie huru kufanya biashara katika mitaa yao. Ufafanuzi huo uliambatana na kutaja sifa za mjasiriamali au mmachinga anayefaa kupewa hicho kitambulisho. Mjasiriamali mwenye sifa ya kupewa kitambulisho cha ujasiriamali ni yule mwenye mauzo yasiyozidi shilingi elfu kumi na moja (11,000) kwa siku ama shilingi milioni Nne (4,000,000) kwa mwaka, yule ambaye yupo kwenye biashara ambayo sio rasmi au eneo lisilo rasmi mfano wamachinga. Pia mafundi pikipiki, wapiga debe, vinyozi ambao saluni zao gharama ya kunyoa na huduma zingine hazizidi shilingi elfu tano. Halmashauri ya mji wa Babati imepokea jumla ya vitambulisho elfu saba ambavyo tayari vimeanza kugawiwa kwa watendaji wa vijiji na hatimaye viwafikie wananchi walengwa. 

Baada ya ufafanuzi mzuri kutoka kwa Afisa Biashara, mheshiwa mkuu wa Wilaya akaeleza juu ya muitikio wa wajasiriamali wadogo wadogo katika kumuunga mkono mheshimiwa Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa kuchangia shilingi za Kitanzania elfu ishirini (20,000) kununua vitambulisho hivyo vya awamu ya kwanza ambavyo hivi sasa vimeisha muda wake. 

Nawapongeza sana kwa kitendo cha kizalendo kumuunga mkono mheshimiwa Rais kwa kuweza kuchangia sh. 20,000 kwa ajili ya vitambulisho ambazo kwa kweli nina imani kubwa zimefanya maendeleo katika taifa letu la Tanzania.

Pia mheshimiwa mkuu wa Wilaya aliendelea kuwapongeza wajasiriamali wadogo wadogo na wamachinga wote wa mji wa Babati kwa shughuli zao za kijasiriamali wanazozifanya kila siku bila bugdha yoyote kwani wameweza kuufanya mji wa Babati kuchangamka na kupendeza machoni mwa kila mtu. 

Nawapongeza sana wamachinga na wajasiriamali wadogo wadogo wote kwa umoja wenu na shughuli zenu za ujasiriamali kwani mmefanya mji wetu wa Babati kuchangamka na kurahisisha upatikanaji wa Bidhaa na mahitaji mbalimbali kwa wananchi, hivyo mimi rai yangu kwenu sasa na mwaka huu tuchangie hiyo elfu ishirini (20,000) kama jinsi serikali yetu ilivyotuomba  na kutuagiza tununue na tusisumbuliwe katika kutoa au kulipa kodi nyingine yoyote, hiyo elfu ishirini inatosha. amesema mheshimiwa mkuu wa Wilaya.

Kwa picha zaidi bonyeza kituo cha habari kwenye menyu.

Imeandikwa na Nyeneu, P. R

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Muendelezo wa Ziara ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati Kata kwa Kata katika Halmashauri.

    June 23, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Babati imetembelewa na Maafisa kutoka Skuli ya Bububu Zanzibar

    June 23, 2025
  • Mafunzo yametolewa kwa wanufaika wa mikopo Awamu ya Tatu katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Babati.

    June 21, 2025
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati amefanya ziara katika Kata ya Bonga.

    June 20, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati