• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Utoaji wa Leseni ya Biashara
    • Utoaji wa Leseni za Vileo
    • Utoaji wa Kibali cha Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Waziri Kairuki atoa angalizo utekelezaji mradi wa BOOST

Imechapishwa: December 13th, 2022

Na Nyeneu, P. R - Arusha

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Angellah J. Kairuki amewataka Viongozi wa Sekretarieti za Mikoa, Viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na wajumbe wa timu za utekelezaji wa mradi wa BOOST kuhakikisha wanasimamia kwa ufanisi utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa elimu ya Awali na Msingi ili kufikia malengo ya serikali ya kutatua changamoto za elimu nchini.

Mhe. Kairuki ameyasema hayo leo Disemba 13, 2022 wakati akifungua Mafunzo ya kuwajengea uwezo Makatibu Tawala wa Mikoa, Maafisa Elimu wa Mikoa, Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na wajumbe wa timu za utekelezaji wa mradi wa BOOST katika Mikoa ya Singida, Manyara na Arusha, uliofanyika Jijini Arusha.

“Serikali inapimwa kwa vigezo katika kutekeleza Mradi wa BOOST nchini, sitakuwa tayari kuona fedha zimetolewa kiasi cha shilingi trilioni 1.15 na kupelekwa katika Mamlaka za Serikali za Mitaa lakini miradi haitekelezwi kwa wakati na fedha hizo kurudishwa, tutakuwa hatujatenda haki kwa wananchi” amesisitiza Waziri Kairuki

Waziri Kairuki amewataka Wajumbe wa mradi huo kuhakikisha fedha zinazotolewa katika utekelezaji wa miradi zinakamilisha miradi iliyopangwa ili kuepusha miradi mingi kutokukamilika huku fedha zikiwa zimekwisha. Vilevile amewataka wajumbe hao kuhakikisha wanaimarisha ushirikiano na jamii katika utekelezaji wa mradi, pia kuzingatia sheria, kanuni na miongozo katika utekelezaji wa mradi ili thamani ya fedha iliyotolewa iendane na majengo yatakayojengwa ili kufikia matokeo yaliyokubalika.

Aidha, amewaagiza Wajumbe hao kuwahamasisha wazazi/walezi kuwapeleka watoto wenye umri wa kuanza shule ili waandikishwe na kuanza shule kwa wakati ili kuwaepushia mzigo walimu kwa kulazimika kurudia kufundisha mambo yale yale kutokana na wanafunzi wengine kucheleweshwa kuanza shule.

Mhe. Waziri Kairuki amesema katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali itatoa shilingi bilioni 240 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi, hivyo amewaagiza kusimamia ujenzi huo ili ukamilike kwa wakati kwa kuzingatia miongozo na wajiepushe na migogoro ambayo huchangia kuchelewesha utekelezaji wa miradi.

Matangazo

  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU November 09, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NGAZI YA TATU July 27, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Waziri Kairuki atoa angalizo utekelezaji mradi wa BOOST

    December 13, 2022
  • Mhe. Jenista Mhagama awasisitiza watendaji wa ofisi yake kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma bora kwa wananchi na watumishi wanaowahudumia

    December 04, 2022
  • Maagizo ya DC Twange kwa Watumishi wa Umma na Wafanyabiashara kuhusiana na utoaji wa risiti za EFD

    December 02, 2022
  • Rais Samia azindua miradi miwili mikubwa iliyogharimu Mabilioni ya fedha Mjini Babati

    November 22, 2022
  • Tazama zaidi

Video

Halmashauri ya Mji wa Babati kuelekea miaka 61 ya Uhuru
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati