• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

TASAF yazindua mfumo mpya wa malipo kwa Walengwa

Imechapishwa: December 18th, 2020

Na Nyeneu, P. R - Mjini Babati

“TASAF ipo katika mchakato wa kubadili njia ya malipo kwa walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini ili kuhawilisha ruzuku kwa njia ya kielektroniki na kuondokana na njia ya kulipa taslimu.” Alisema Bw. Edmund Mwalongo (Mwezeshaji kutoka TASAF Makao makuu) kwenye mafunzo ya kuwawezesha wawezeshaji ngazi ya Halmashauri yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Babati. Mafunzo haya yanayofanyika nchi nzima yakiwa na lengo la kuwajengea uwezo wawezeshaji kuwaandikisha walengwa wote katika njia ya malipo kwa mtandao yaani e-Payment ambapo walengwa wanatakiwa kuwa na akaunti za simu au benki.

Mpango huu umetekelezwa kwa majaribio katika maeneo ya mamlaka ya utekelezaji 19 Tanzania Bara na Visiwani ambazo ni asilimia 10 ya mamlaka zote 181 zilizopo. Mamlaka hizo ni Bahi, Kisarawe, Mkuranga, Unguja, Kilwa, Siha, Bagamoyo, Mpanda Mji, Arusha Mjini, Kigoma Manispaa, Songea Manispaa, Muheza, Temeke, Kinondoni, Ilala, Ubungo, Kigamboni, Chalinze na Urambo. Majaribio haya yalianza mwezi Mei/Juni 2017.

Jumla ya walengwa kabla ya uhakiki katika mamlaka hizo walikuwa 101, 568, baada ya uhakiki idadi ya walengwa katika PAA hizo ni 73,911. Ili kuweza kufanikisha zoezi hili la uandikishaji wa Wakilishi, ni lazima mlengwa awe amekizi vigezo vifuatavyo:-

1. Awe mwakilishi wa kaya na sio mkuu wa kaya

2. Awe na akaunti iliyosajiliwa katika huduma ya benki au huduma za kifedha za simu

3. Jina lililosajiliwa katika mpango lifanane na jina lililosajiliwa kwenye akaunti ya simu au benki

4. Ajaze na kusaini fomu ya maombi (concent form) ya kujiunga kupokea malipo kwa njia ya mtandao

5. Akaunti ithibitishwe uhai wake na jina lililosajiliwa katika huduma ya benki au huduma za kifedha za simu.

Aidha, Katika kipindi hiki  uhamasishaji na kuwawezesha  wawakilishi wa kaya ambao hawana akaunti kufungua akaunti  mpya za benki au akaunti za simu ambazo zitawawezesha kupokea fedha  kwa kipindi cha malipo ya  Nov/December umefanyika na unaendelea kufanyika awamu kwa awamu. Takwimu  hizo zitakusanywa na zitahakikiwa ili ziweze kutumika kwa  malipo yajayo yaani yatakayofanyika kwa kipindi cha November/December. Muwezesha aliendelea kusisitiza kuwa utaratibu wa malipo ya kielektroniki uelezwe bayana kwa wawakilishi  wa kaya zote na kujaza fomu ya kujiandikisha(consent form). Hata hivyo, kwa kujaza na kusaini fomu ya uthibitisho wa malipo ya kielektroniki au fomu ya malipo ya kielektroniki, wawakilishi wa kaya watakuwa wamethibitisha na kutoa idhini  ya kulipwa kupitia simu au benki akaunti. Pia watakuwa wamewaruhusu TASAF kuwasiliana na benki au watoa huduma ili kuwaomba  uthibitisho wa taarifa za akaunti zao walizotoa, kwani yote haya yanafanyika kwaajili ya kuimarisha utoaji huduma kwa walengwa.

Pamoja na hayo, utambuzi wa walengwa kwa njia ya vidole (Proper identification/authentication) ni moja ya hitaji muhimu la kufanikisha malipo kwa njia ya OTC(Over The Counter) na ili malipo kwa njia ya OTC yaweze kufanikiwa ni lazma kila mlengwa awe na number ya NIDA yaani amejisajili NIDA. Pia, ili kufanikisha hili, TASAF imekuwa ikishirikiana na NIDA kuhakikisha walengwa wote wanaandikishwa na kupewa number za utambulisho NIN (National Identification Number) hivyo kuwalazimu walengwa wote ambao hawajawasilisha/hawajajiandikisha wanatakiwa kufanya hivyo na NIN zote kwa utaratibu mzuri zitachukuliwa na kuingizwa kwenye mfumo wa e-Payment.

Bw. Malongo aliendelea kutoa mafunzo na kueleza malengo na faida ambazo mlengwa angepata katika malipo kwa njia ya mtandao, kama ifuatavyo;

  • Malipo kwa njia ya mtandao ni njia Salama kabisa katika fedha za mlengwa. Malipo kwa njia ya kielektroniki yataondoa athari zinazoweza kutokea wakati wa kusafirisha fedha taslimu kuelekea maeneo ya malipo

  • Huleta fursa zaidi ya kufanya maamuzi sahihi kabla ya kutumia. Malipo kwa njia ya e-Payment yataleta fursa kwa walengwa kifikiri na kufanya maamuzi sahihi katika matumizi ya huduma za kifedha ili kuboresha maisha yao mfano Kulipia Bima, Kuweka akiba na kulipia huduma mbalimbali.

  • Kupata pesa kwa wakati na popote alipo mlengwa bila kusubiri na kupanga foleni. Hii itawawezesha walengwa kupokea pesa moja kwa moja katika akaunti zao za simu au benki, mahali popote walipo bila kusubiri na kupanga foleni.


  • Kupata muda zaidi wa kufaya shughuli za maendeoleo

  • Pia kupunguza gharama za kusafirisha fedha kwa magari kuelekea maeneo ya malipo.

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Timu ya Menejimenti Halmashauri ya Mji Babati imefanya Ziara kukagua Miradi ya Maendeleo

    May 07, 2025
  • Watumishi Manyara wametakiwa kupendana na kuacha chuki.

    April 30, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe.Emmanuela Kaganda amewataka Wananchi kuuenzi Muungano.

    April 26, 2025
  • Chanjo nyongeza ya polio (IPV2) kuanza kutolewa kwa watoto wa miezi 9 mwezi wa tano 2025.

    April 24, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati