• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumisha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Sekta ya Elimu Babati Mji yanufaika na NMB

Imechapishwa: May 9th, 2022

Imeandikwa na Nyeneu, P. R

Mhe. Pauline Gekul, Naibu Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini, leo tarehe 09 Mei 2022, amehudhuria hafla fupi ya makabidhiano ya Kompyuta kwa shule za Mji wa Babati kutoka Benki ya NMB. Makabidhiano ya vifaa hivyo yaliyowakutanisha Waheshimiwa Madiwani, Maafisa Elimu Msingi na Sekondari, Maafisa Elimu kata, Wakuu wa Shule Msingi na Sekondari yamefanyika katika shule ya Msingi Babati iliyopo Kata ya Bagara ambapo Mbunge huyo alikuwa ndiye mgeni rasmi.

Mhe. Gekul ameipongeza Benki ya NMB kwa kuwa mstari wa mbele katika juhudi za maendeleo kwa kusaidia jamii zetu kwani jamii hizi ndio zimeifanya benki ya NMB kuwa hapa ilipo na kubwa kuliko benki yoyote hapa nchini. "Kwahiyo watu wa NMB ninyi mmekuwa marafiki wema kwetu wa Jimbo hili, mmekuwa mkitupokea lakini mmekuwa mkitusaidia. Mimi ninawashukuru kama Mbunge wa Jimbo kwa niaba ya wananchi hawa", alisisitiza Mhe. Gekul

Aidha, Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini Bw. Dismas Prosper katika hotuba yake amesema kuwa changamoto za sekta ya elimu Tanzania kwa benki ya NMB ni jambo la kipaumbele, hii ni kutokana na ukweli kwamba elimu ndio ufunguo mkuu wa maendeleo kwa taifa lolote hapa duniani. "Tunatambua juhudi za Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan za kusimamia upatikanaji wa elimu bora kwa nguvu zote kwa kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma hizi mjini na vijijini; hatuna budi kuipongeza Serikali kwa hilo", Aliongezea Bw. Dismas. 

Benki ya NMB leo imeweza kukabidhi jumla ya Kompyuta za mezani 25 kwa shule za Msingi 09 ambazo ni Gendi, Maisaka, Darajani, Hangoni, Malangi, Himiti, Managha, Oysterbay na Babati na kwa shule za Sekondari 10 ambazo ni Nakwa, Bagara, Sigino, Kwaraa, Bonga, Himiti (Gekul), Kololi, Kwaang'w, Mutuka na Hangoni. Bw. Dismas amewaasa waliopokea vifaa hivyo kuwa kompyuta hizo zitatumika vyema kwaajili ya kuwajenga vijana na kuwapa mwanga fasaha wa kidigitali kwani ndiko ulimwengu unakoelekea. Hivyo ni vyema kuanza kuwaandaa vijana wetu na vifaa hivi vya kidigitali katika masomo yao.

Sambamba na hayo, Bw. Dismas amemalizia kwa kusema kuwa Benki ya NMB itaendelea kuunga mkono juhudi za wadau wake wakubwa katika kuhakikisha kuwa changamoto za jamii zinapatiwa ufumbuzi katika kuboresha huduma za elimu.


Matangazo

  • TANGAZO LA AJIRA ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022 May 05, 2022
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 BABATI MJI December 18, 2020
  • ORODHA YA WASIMAMIZI WA VITUO, WASIMAMIZI WASAIDIZI WA VITUO NA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA October 20, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA September 21, 2020
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Sekta ya Elimu Babati Mji yanufaika na NMB

    May 09, 2022
  • Maelekezo ya utekelezaji wa Mtaala - Kutoka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia

    February 03, 2022
  • Mradi wa madarasa 18 uliogharimu Tshs. 379,267,500 wakabidhiwa

    December 28, 2021
  • RC MAKONGORO APONGEZA MWENENDO MZURI WA MIRADI YA MADARASA

    November 30, 2021
  • Tazama zaidi

Video

Karibu Mwenge wa Uhuru 2022 Mkoani Manyara
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati