• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Utoaji wa Leseni ya Biashara
    • Utoaji wa Leseni za Vileo
    • Utoaji wa Kibali cha Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

RCCE yajengewa uwezo wa kufikisha elimu ya Afya kwa Umma

Imechapishwa: April 28th, 2023

Na Nyeneu, P. R - Mjini Babati

Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Jacob Twange amewataka wajumbe wa kamati ya uelimishaji, uhamasishaji na ushirikishaji jamii (RCCE) ngazi ya Wilaya, kuhakikisha kuwa lile jukumu lao la Msingi la kuwa Daraja kati ya Watalaam Kwenda kwa Wananchi linatekelezwa kikamilifu. DC Twange ameyasema hayo akiwa mgeni rasmi katika kikao maalumu cha kuwajengea uelewa wajumbe hao katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko na magonjwa mengine. “Lengo mama ni lilelile la kuendelea kutii maelekezo ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan la kulinda Afya za Wananchi wake ili shighuli za Maendeleo na kukuza uchumi ziendelee vizuri”. Alisisitiza DC twange.

Vilevile Mtaalamu kutoka Wizara ya Afya Idara ya Kinga sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma, Bi. Magdalena Dinawi amesema lengo kuu la kuunda kamati hii ni kuwezesha kufikisha elimu ya Afya kwa Umma kwaajili ya kuzuia magonjwa ya Mlipuko na magonjwa mengine. Baadhi ya Majukumu ya Kamati hii ni Kuwezesha, kusimamia na kusaidi kamati za Wilaya kutoa elimu ya Uchanjaji na Elimu ya Afya kwa jamii. Pia Kusambaza vipeperushi na jumbe mbalimbali kwa jamii ilioko kwenye hatari, Kusaidia na kuwezesha jamii kushiriki katika shughuli mbalimbali wakati wa majanga na dharura za afya. “Tumeona tushirikishe jamii ili kuweza kufikisha ujumbe kwa haraka”. Alieleza Mtaalamu

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Bi. Anna Fisoo amewaasa viongozi wa Dini na wataalamu wa Tiba Mbadala kuwa na mtandao wa rufaa. Pale inapotokea muumini au mgonjwa ameonekana na dalili za ugonjwa wa mlipuko mfano kipindupindu basi apelekwe au aelekezwe kufika kwenye kituo cha kutolea huduma za Afya ambacho kipo karibu ili kuzuia athari zaidi kwa wengine. Pia amewaomba wataalamu kutoka Wizara ya Afya kuendelea kutoa ushirikiano wao pale watakapohitajika katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zitakazojitokeza.

Kamati hii ya uelimishaji, uhamasishaji na ushirikishaji jamii inaundwa na Mkuu wa Wilaya ambaye ndiye Mwenyekiti, Mganga Mkuu wa Halmashauri ambapo huyu ni katibu wa kamati na atakuwa na jukumu la kumpa ushauri wa kitalaam Mwenyekiti wa kamati. Mratibu wa elimu ya afya kwa umma wa Halmashauri, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, Afisa Elimu wa Wilaya.

Baadhi ya Wajumbe wengine ni Afisa kilimo na Afisa Uvuvi wawili, Afisa Biashara, Mratibu wa huduma za afya ngazi ya jamii, Mratibu wa elimu ya Afya Shuleni, Afisa Afya wa Halmashauri, Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri, Afisa Habari wa Halmashauri. Pia, Afisa utamaduni na michezo wa Halmashauri, Wawakilishi wa Tiba Asili na Tiba Mbadala, Mratibu wa chanjo wa Halmashauri, Kiongozi wa kijamii (mwanaume na mwanamke), Viongozi wa Dini kutoka katika madhehebu mbalimbali yaliyopo kwenye eneo husika, Waandishi wa Habari n.k.

Matangazo

  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU November 09, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NGAZI YA TATU July 27, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Mhe.Queen Sendiga amefanya kikao na madereva wa bodaboda,bajaji.machinga na mama lishe Mkoani Manyara.

    September 20, 2023
  • Mhe.Queen Sendiga ameweka jiwe la msingi katika shule ya mpya ya Awali na Msingi

    September 15, 2023
  • Mhe. Joyce Ndalichako amekagua maandalizi ya Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 Mkoani Manyara.

    August 28, 2023
  • Bi.Pendo Mangali amezindua ( PJT-MMMAM) ngazi ya Halmashauri ya Mji wa Babati

    August 22, 2023
  • Tazama zaidi

Video

Halmashauri ya Mji wa Babati kuelekea miaka 61 ya Uhuru
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati