• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Utoaji wa Leseni ya Biashara
    • Utoaji wa Leseni za Vileo
    • Utoaji wa Kibali cha Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Rais Samia azindua miradi miwili mikubwa iliyogharimu Mabilioni ya fedha Mjini Babati

Imechapishwa: November 22nd, 2022

Na Nyeneu, P. R

Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili Mkoani Manyara Mjini Babati leo tarehe 22 Mwezi Novemba 2022 ikiwa ni ziara yake ya kikazi ya siku mbili na ya kwanza Mkoani humo na kupokelewa kwa shamra shamra kubwa na Wananchi wa Mji wa Babati.

Katika ziara yake, Mhe. Rais amezindua mradi wa Maghala na Vihenge vya kuhifadhia Chakula vinavyosimamiwa na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) vilivyopo Mjini Babati katika Kata ya Maisaka Kijiji cha Malangi. Mradi huu umegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 19 hadi kukamilika. Naye Mhe. Bashe, Waziri wa Kilimo katika maelezo yake amesema kuwa malengo ya Wizara hadi kufikia mwishoni mwa Mwaka 2023 uwezo wa Nchi wa kuhifadhi nafaka ufikie tani laki tano (tani 500,000).

“Malengo yetu kufika mwezi Disemba mwaka kesho Mhe. Rais, uwezo wa nchi kuhifadhi nafaka ufike tani laki 5. Sasa hivi ulitupatia fedha tunauwezo wa kununua mazao zaidi ya tani 201,400” Akieleza zaidi Mhe. Bashe.

Aidha, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la msingi la uzinduzi wa mtandao wa Barabara za lami Mjini Babati wenye urefu wa kilomita Nane nukta moja (kilomita 8.1). Halmashauri ya Mji Babati imeweza kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya Barabara, na Kilomita 8.1 zimekamilika hadi sasa na kugharimu jumla ya shilingi Bilioni 12 kwenye miundombinu pekee (Barabara, Mitaro ya maji ya mvua, Taa za barabarani 182 na njia za waenda kwa miguu), gharama za usimamizi ni shilingi Bilioni 1 na hivyo  kufanya jumla ya gharama za ujenzi kuwa ni zaidi ya shilingi Bilioni 13.

Vilevile Mhe. Rais ameeleza kuwa dhamira ya Serikali ni kuendelea kuboresha miundombinu katika mji wa Babati. “Lakini mbali na uzinduzi, kuna mradi mkononi tunauchakata ambapo Babati Mji Mtapata tena Kilomita tano za lami. Tunataka Mji wa Babati uwe Mji kweli kweli, watu wafanye Biashara usiku na mchana na Mji uwe na hadhi ya Mji kweli kweli”. Amesisitiza Mhe. Rais.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Bi. Anna Fisoo kwa niaba ya Wananchi wa Mji huo, amemshukuru sana Mhe. Rais Samia Suluhu kwa kuipatia fedha Halmashauri hiyo kwaajili ya utekelezaji wa mradi huu ambapo awali uliwekwa Jiwe la Msingi mwaka 2016 na Mhe. Rais Samia Suluhu akiwa Makamu wa Rais.

Katika taarifa yake, Kaimu Mkurugenzi ameelezea namna mradi ulivyowanufaisha wananchi na kusema kuwa Mradi umewanufaisha wananchi wa Mji wa Babati na kuondoa adha ya vumbi na kupunguza adha ya mafuriko katakati ya Mji Babati na kuinua thamani ya ardhi katika Mitaa ya Oysterbay, Nyunguu, Mji Mpya, Babati Mjini na Maisaka B katika Kata za  Babati na Bagara. Vilevile mradi umeongeza usalama wa waenda kwa miguu kutokana na kuwepo kwa taa za barabarani zinazoangaza wakati wa usiku na pia umewezesha kuongeza muda wa biashara ndani ya maeneo ya biashara na makazi.

Ikumbukwe kuwa, Halmashauri ya Mji wa Babati ni mojawapo ya Halmashauri 18 zilizopata fedha za Benki ya dunia na kutekeleza mradi wa kuzijengea mamlaka za serikali za Mitaa kuboresha Miji na Manispaa na Majiji nchini Tanzania ULGSP na kusimamiwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Matangazo

  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU November 09, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NGAZI YA TATU July 27, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Miaka Miwili ya Rais Samia Manyara ni Shangwe tupu

    March 18, 2023
  • Waziri Kairuki atoa angalizo utekelezaji mradi wa BOOST

    December 13, 2022
  • Mhe. Jenista Mhagama awasisitiza watendaji wa ofisi yake kuwa na kauli nzuri na kutoa huduma bora kwa wananchi na watumishi wanaowahudumia

    December 04, 2022
  • Maagizo ya DC Twange kwa Watumishi wa Umma na Wafanyabiashara kuhusiana na utoaji wa risiti za EFD

    December 02, 2022
  • Tazama zaidi

Video

Halmashauri ya Mji wa Babati kuelekea miaka 61 ya Uhuru
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati