• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Mradi wa madarasa 18 uliogharimu Tshs. 379,267,500 wakabidhiwa

Imechapishwa: December 28th, 2021

Na Nyeneu, P. R

Halmashauri ya Mji wa Babati kupitia mradi namba 5441 – TCRP hadi sasa imepokea kiasi cha Tshs. 778,515,998.08 ambapo Tshs. 28,515,998 ni kwa ajili ya uhamasishaji wa chanjo na Tshs. 750,000,000 kwaajili ya miradi ya miundombinu katika sekta ya Elimu na Afya. Katika fedha hizo, Tshs. 360,000,000 ni kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 18 sekta ya Elimu Msingi na Sekondari, Tshs. 300,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa dharura katika Hospitali ya Mji wa Babati (Emergency Medical Department) na Tshs. 90,000,000 kwaajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi 3 kwa 1 (three in one) kituo cha Afya Mutuka. 

"Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya; Ujenzi wa madarasa 18 umegharimu Tshs. 379,267,500 zikiwemo Tshs. 360,000,000 za Mradi na Tshs. 19,267,500 ikiwa ni Nguvu za wananachi kwa shule za sekondari za Kwaang’w (01), Mutuka (01), Sigino (01), Bonga (01), Bagara (01), Kwaraa (01), Nangara (01), F.T. Sumaye (01), Babati Day (02), Nakwa (02), Hangoni (02), Komoto (02) na vyumba viwili vya madarasa katika shule shikizi ya Sora. Ujenzi wa miundombinu hii ulianza tarehe 04.12.2021 na kukamilika kwa asilimia 100 tarehe 17.12.2021". Amesema hayo Kaimu mkurugenzi wa Mji Ndg. Faustine Masunga wakati akisoma taarifa ya makabidhiano ya mradi huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Jacob Twange leo 28 Desemba 2021.

Katika kuwezesha utekeleaji wa mradi namba 5441 – TCRP, Halmashauri ya Mji wa Babati ilifuata hatua mbalimbali ikiwemo kuunda Kamati ya Uratibu ya Halmashauri, pia kufanya kikao cha bodi ya zaburi kuridhia mchakato wa manunuzi wa “force account” na “single source”, kufanya kikao cha kamati ya fedha na uongozi kwa niaba ya baraza la madiwani na kuridhia mpango. VIlevile kuhamasisha Baraza la madiwani kuhusu mpango na limepatiwa mafunzo rejea ya “force account”, kuunda Kamati za uratibu za Kata na kupatiwa mafunzo rejea ya “force account” na pia kuunda Kamati za miradi za “force account” katika ngazi ya Shule.

Aidha, Halmashauri ya Mji wa Babati kwa mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa imepokea fedha toka serikali kuu jumla ya Tshs. 1,087,500,000 kwa ajili ya ujenzi ya miundombinu ya sekta ya Afya na Elimu. Ambapo Tshs. 50,000,000 ni kwaajili ya ujenzi wa jengo la Utawala shule ya Sekondari Komoto ikiwa ni awamu ya kwanza, kiasi cha Tshs. 387,500,000 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Maabara 04, Ujenzi wa Madarasa 11 katika sekta ya Elimu. Katika sekta ya Afya kiasi cha Tshs. 700,000,000 zilipokelewa kwa ajili ya uendelezaji wa ujenzi wa Zahanati ya Sigino, Chemchem na  vituo vya Afya Singe, Mutuka, Singu na Maisaka.

Katika taarifa ya makabidhiano mheshimiwa mkuu wa Wilaya amesomewa faida na changamoto za mradi Namba 5441-TCRP. Faida mojawapo ya ukamilikaji wa Mradi 5441 – TCRP utasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani na kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. Vilevile changamoto zilikuwa ni ucheleweshwaji wa saruji mifuko 600 ambayo ilinunuliwa kwa pamoja (Bulk Purchase) kiwanda cha Dangote na pia kupanda kwa bei ya vifaa vya ujenzi hususan vioo, Bati na Nondo.

Mheshimiwa DC amekabidhiwa rasmi jumla ya madarasa 18 ambapo kwa Shule za Sekondari ni madarasa 16 na Shule Shikizi madarasa 02 pamoja na Meza na Viti 1,600 na madawati 30 kwa ajili ya hatua zaidi.

Picha zote na Azael Amani

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Timu ya Menejimenti Halmashauri ya Mji Babati imefanya Ziara kukagua Miradi ya Maendeleo

    May 07, 2025
  • Watumishi Manyara wametakiwa kupendana na kuacha chuki.

    April 30, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe.Emmanuela Kaganda amewataka Wananchi kuuenzi Muungano.

    April 26, 2025
  • Chanjo nyongeza ya polio (IPV2) kuanza kutolewa kwa watoto wa miezi 9 mwezi wa tano 2025.

    April 24, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati