• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na utumishi
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango Miji
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi
      • Usafi na Mazingira
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Utoaji wa Leseni ya Biashara
    • Utoaji wa Leseni za Vileo
    • Utoaji wa Kibali cha Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Fomu za Maombi
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Miaka 59 ya Muungano Umoja na Mshikamano ndio Nguzo ya Kukuza Uchumi Wetu

Imechapishwa: April 26th, 2023

Na Nyeneu, P. R -  Gallapo

Kufuatia maelekezo ya serikali kuwa maadhimisho ya sherehe za Muungano kwa mwaka huu zifanyike katika ngazi ya Mikoa nchini kote, Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Charles Makongoro Nyerere leo tarehe 26 Aprili, 2023 ameungana na wananchi wa Mkoa huo kuadhimisha kilele cha sherehe za miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika Katika Kijiji cha Gallapo Wilayani Babati ambapo kauli mbiu ni “Umoja na Mshikamano ndio Nguzo ya Kukuza Uchumi Wetu”.

Maadhimisho haya ambayo yameanza kufanyika kuanzia tarehe 17 Aprili, 2023 yaliambatana na shughuli mbalimbali za kijamii hususan upandaji miti, usafi wa mazingira na mashindano ya michezo na sanaa mbalimbali. Kadhalika, yaliambatana na Mashindano ya uandishi wa Insha kwa shule za Msingi na Sekondari na washindi washindi wa katika mashindano mbalimbali wamezawadiwa vyeti na fedha taslimu.

“Lengo kuu la Muungano huu ilikua ni kuendelea kudumisha uhusiano baina ya pande hizi mbili ambao umekuwepo kwa muda mrefu katika nyanja mbalimbali kama vile undugu wa damu, biashara, utamaduni, lugha na mahusiano ya karibu ya kisiasa baina ya vyama vya TANU na ASP ambavyo baadae viliunda Chama Cha Mapinduzi”. Alielezea Mhe. RC.

Vilevile Mhe. Makongoro amewapongeza sana wananchi wa Mkoa wa Manyara kwa kuuenzi Muungano kwa vitendo kwa kuimarisha Mshikamano, Ulinzi na Usalama unaowezesha watu wote kufanya kazi za uzalishaji mali kwa amani na utulivu na hivyo kukuza uchumi wa Mkoa na Nchi kwa ujumla.

Lakini pia amewapongeza kwa kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza miradi ya maendeleo ambapo hadi sasa Mkoa umefanikiwa kuimarisha utoaji wa huduma za kijamii na kiuchumi kama vile Kuongeza idadi ya Shule za Msingi na Sekondari ambapo hadi sasa Mkoa una jumla ya Shule za Msingi 642 na Sekondari 154, Kuongeza idadi ya vituo vya kutolea huduma za Afya mwaka hadi mwaka ambapo hadi sasa Mkoa una jumla ya Zahanati 186, Vituo vya Afya 29, na Hospital 12; Aidha, hali ya upatikanaji wa dawa muhimu imefikia 91%

Pia, Mhe. Mkuu wa Mkoa amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake mahiri ambapo ameendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Mkoa.

Matangazo

  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU November 09, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NGAZI YA TATU July 27, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Mamilioni ya fedha za BOOST kuboresha Sekta ya Elimu Msingi na Awali Babati Mji.

    May 09, 2023
  • RCCE yajengewa uwezo wa kufikisha elimu ya Afya kwa Umma

    April 28, 2023
  • Miaka 59 ya Muungano Umoja na Mshikamano ndio Nguzo ya Kukuza Uchumi Wetu

    April 26, 2023
  • Halmashauri zahimizwa kuendelea kupanda miti ili kufikia lengo la Mwaka la Mkoa

    April 25, 2023
  • Tazama zaidi

Video

Halmashauri ya Mji wa Babati kuelekea miaka 61 ya Uhuru
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati