Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan amehitimisha Kilele cha Mbio za Mwenge Uhuru 2023 Mkoani Manyara shughuli hiyo imehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu Wa Rais,Mawaziri, Naibu Waziri Mkuu pamoja na Spika wa Bunge, katika shughuli hiyo kubwa ya kitaifa.Ambapo Mwenge wa Uhuru umekimbizwa katika Halmashauri 195 na Mikoa 31 Tanzania Bara na Visiwani.
Mhe. Dk.Samia Suluhu Hassan amehudhuria Misa Takatifu ya kumuombea Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Kanisa la Roho Mtakatifu Mjini Babati.Pia ametembelea maonesho ya wiki ya Vijana Kitaifa ambayo yamefanyika katika eneo la Stendi ya zamani na kuhudhuriwa na vijana takribani 450 kutoka Mikoa yote Tanzania Bara pamoja na Visiwani.
Pia Mhe. Rais amesisitiza kuziishi falsafa za Mwalimu Nyerere na kutozipuuza, ametaka kudumisha Umoja ikiwa ni moja ya falsafa ambazo Mwalimu Nyerere alihimiza katika maisha yake. Ameongeza kuwa Serikali imeweka jitihada za kuboresha maisha ikiwemo Ujenzi wa Vyuo ya Veta lengo ni Vijana kupata ujuzi na amewapongeza Vijana ambao walioshiriki katika wiki ya Vijana Kitaifa.
Vilevile amezikumbusha Halmashauri na wananchi kupanda miti na kutochoma moto ovyo mashambani kwa kufanya hivyo kunasababisha mabadiliko ya tabia ya nchi. Pia amepongeza Taasis zinazofanya kampeni juu ya upandaji miti na utunzaji wa mazingira.Na amesisitiza mashindano juu ya upandaji miti yaendelee ili kuhamasisha zoezi la upandaji miti na kutunza mazingira sambamba na Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2023 Mabadiliko ya Tabia ya Nchi”Tunza mazingira,Okoa vyanzo vya Maji kwa ustawi wa Viumbe Hai kwa Uchumi wa Taifa.
Pia Mhe. Dk.Samia Suluhu Hassan amewataka Viongozi kuwashauri wananchi kuacha kilimo cha zao la bangi na kulima mazao ya biashara au kufanya nyingine tofauti na hizo za madawa ya kulevya hakina tija na kinaleta madhara kwa Taifa.. Sambamba na hilo amewataka wananchi kuchukua tahadhari kubwa juu ya ugonjwa wa Ukimwi, amesisitiza kuhusu umuhimu wa lishe huku akiwataka Wakuu wa Mikoa kulishughulikia suala hilo na ametoa takwimu za Mikoa ambayo inakabiliwa na changamoto ya udumavu na kutaka Viongozi kufanyia kazi suala hilo.
Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amemshukuru Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassan kwa miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Manyara na matukio yote matatu Kumbukizi ya Mwalimu Nyerere na kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 pamoja na wiki ya vijana Kitaifa .Ameeleza kuwa kufanyika kwa mambo imesaidia kuleta mzunguko wa fedha Mkoa wa Manyara.
Vilevile Mhe.Joyce Ndalichako Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu amesema kuwa Mkoa wa Manyara una miradi katika Sekta ya Afya,Elimu,Kilimo na Maji takribani Millioni 12 katika mradi wa maji Sigino,Mradi wa ujenzi wa soko la Madini Millioni 5.4,mradi wa Shule ya wasichana Mkoa wa Manyara Billioni 3 na mradi wa Kilimo cha umwagiliaji Millioni 11.3.
Barabara ya Babati - Singida
Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati
Nukushi: +255-027-2510095
Simu: +255-027-2510095
Barua pepe: td@babatitc.go.tz
Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati