• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Mfumo wa Kugawa Mapato ya 10% ya Halmashauri kwa Makundi Maalum

Imechapishwa: November 13th, 2022

Na  Nyeneu, P. R

Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, imeanza rasmi kutumia mfumo wa kieletroniki wa kutoa mikopo ya asilimia 10 inayotokana na makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na watu wenye ulemavu. Halmashauri ya Mji wa Babati, imetenga fedha shilingi 155,741,173.70 ikiwa ni asilimia kumi (10%) kutoka kwenye makusanyo ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo ya masharti nafuu kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu.

Ili kuweza kuomba mikopo hii, waombaji wanatakiwa wawe na sifa zifuatazo; Kwanza kwa Vijana Wajasiriamali wawe na umri wa miaka 18 hadi 35, Wanawake wajasiriamali wawe na umri miaka 18 na kuendelea. Watu wenye ulemavu Wajasiriamali wa na umri kunzia miaka 18 na kuendelea. Waombaji wa mikopo wawe wakazi wa Halmashauri husika ambapo kwa Babati Mjini, wawe ni wakazi wa Halmashauri ya Mji wa Babati, Waombaji wote wa mikopo wanapaswa kuwa raia wa Tanzania, pia wawe wamejiunga katika vikundi vya watu 5 - 30. Kwa muombaji mjasiriamali mwenye ulemavu asiye kwenye kikundi atapaswa awe na leseni ya biashara na hati ya utambulusho kutoka halmashauri ya Mji wa Babati. Watu wenye ulemavu wasio na leseni watajiunga kuanzia watatu na kujisajili kupitia mfumo na kupata hati ya utambulisho.

Aidha, vikundi vyote vinapaswa kuomba mkopo kwa kupitia mfumo wa maombi ya Mikopo ya asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kutumia kiunganishi https://mikopohalmashauri.tamisemi.go.tz, huu ni mfumo rasmi ambao umetengenezwa na kuratibiwa na OR – TAMISEMI. Pia waombaji wote wa mikopo wafike kwa Afisa Maendeleo ngazi ya Kata kwa maelezo zaidi.

Viambatisho vinavyohitajika

  • Barua ya Maombi ya Mkopo
  • Nakala ya katiba
  • Andiko la Mradi/Mpango wa Biashara
  • Nakala za vitambulisho vya taifa
  • Barua za wadhamini na picha za vikundi
  • Picha za passport size.
  • Hati ya Usajili

Faida za Mfumo

  • Matumizi ya mfumo huu utatusaidia sana kuongeza uwazi wa uombaji, utoaji na urejeshaji wa mikopo hiyo.
  • Mfumo utasaidia kuongeza uwajibikaji, usawa na uadilifu katika kutoa huduma ya mikopo kwa vikundi husika na kusaidia kuwa na takwimu sahihi na kurahisisha utoaji wa mikopo kwa wakati

Aidha, Wananchi wote wa Halmashauri ya mji wa Babati wanahimizwa kutumia fursa hii ya mikopo ili kujikwamua kiuchumi kwa kutuma maombi yao ndani ya muda wa siku 14 kuanzia tarehe 09/11/2022 na mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 16/11/2022 saa tisa na nusu alasiri (9:30).

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Muendelezo wa Ziara ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati Kata kwa Kata katika Halmashauri.

    June 23, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Babati imetembelewa na Maafisa kutoka Skuli ya Bububu Zanzibar

    June 23, 2025
  • Mafunzo yametolewa kwa wanufaika wa mikopo Awamu ya Tatu katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Babati.

    June 21, 2025
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati amefanya ziara katika Kata ya Bonga.

    June 20, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati