• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Bodi ya Huduma za Afya yazinduliwa

Imechapishwa: May 10th, 2021

Na Nyeneu, P. R

Katibu Tawala Wilaya ya Babati Ndg. Halfan Matipula ameziasa Bodi na kamati ya Huduma za Afya ikiwa tu baada ya uzinduzi kuwa jukumu lao kubwa ni kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa kiwango kwa mujibu wa huduma zilizopangwa kutolewa kwenye maeneo husika. Ameyasema hayo leo tarehe 10 Mei 2021 akiwa mgeni rasmi kumuwakilisha Mkuu wa Wilaya Mhe. Jacob Twange katika uzinduzi wa bodi ya huduma za afya katika Halmashauri na kamati ya usimamizi wa Hospitali. 

"Kwahiyo ninyi mnapaswa kusimamia huduma zilizopangwa kutolewa kwenye kituo cha afya, hospitali zetu zinatolewa kwa viwango ili kupunguza malalamiko ya Wananchi kwa serikali. Hilo ndo jambo la Msingi kwa sababu Serikali kuu haiwezi kusimamia kila kitu".

Aidha, Katibu Tawala amesema kuwa Mhe. Rais yeye anasema kati ya vitu ambavyo hapendi sana kuviona ni mabango ya wananchi yanayoashiria utoaji mbovu wa huduma kwa wananchi. Hivyo basi, bodi na kamati hizo zihakikishe wananchi wanapata huduma zinazotakiwa.

Katika utekelezaji wa lengo la kuboresha huduma za afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, ilitungwa sheria ya kuwashirikisha wananchi katika kusimamia huduma za Afya pamoja na kuzipa Halmashauri Mamlaka ya utekelezaji wa maboresho hayo. Maboresho yanalenga Kuhamasisha na kushirikisha Jamii katika kubuni, kupanga, kutekeleza na kutathmini mipango ya Afya. Vilevile Kuziongezea Halmashauri madaraka na uwezo wa kuamua na kusimamia vyanzo vya mapato kama vile iCHF na NHIF. Hii itasaidia kupunguza pengo la mapato lililopo katika sekta ya Afya. 

"Bodi na Kamati zitadumu kwa miaka 3 na Bodi inapovunjwa au kumaliza kipindi chake, itakasimu madaraka yake kwa CHMT na pia Kamati ya Usimamizi ya Hospitali ikivunjwa au kumaliza kipindi chake, timu ya Uendeshaji Huduma za Afya ya Hospitali (HMT) itakasimu madaraka ya Kamati". Alisema Mganga Mkuu wa Halmshauri ya Mji Babati Dkt. Halima Mangiri

Hivyo basi, kwa mujibu wa sheria hiyo Halamashauri zimepewa mamlaka ya kuunda Bodi za Afya za Halmashauri na Kamati za Vituo vya kutolea huduma za Afya, ambapo kamati hizo zinahusishwa wajumbe wafuatao:-

  1. Wawakilishi wa watumia huduma (wananchi)
  2. Wawakilishi wa vituo vya mashirika ya dini
  3. Mashirika yasiyo ya serikali
  4. Vituo vya watu binafsi
  5. Mwakilishi wa Madiwani
  6. Vituo vya huduma vya serikali vya ngazi ya chini na 
  7. Wataalamu/Secreteriate.

Bodi hizo za afya na kamati za vituo vya kutolea huduma za afya zinakuwa na majukumu yafuatayo.

  1. Kujadili na kushauri juu ya mipango ya Afya na bajeti (Kamati – Hospitali ) na kuidhinishwa na Halmashauri
  2. Kupokea , kuchambua na kuidhinisha taarifa za utekelezaji wa idara kutoka  CHMT ( Kamati ya Hospitali - HMT)
  3. Kubuni vyanzo vya mapato (kamati - Hospitali)
  4. Kusaidia CHMT katika kusimamia rasilimali za Vituo (Kamati – HMT)
  5. Kushikiana  na Kamati za Vituo, Sekta binafsi na wadau  wengine katika kuinua kiwango cha Afya na utoaji wa huduma
  6. Kusimamia miundombinu ya Afya
  7. Kuaandaa na kutekeleza mpango kazi
  8. Kufanya shughuli za ufuatailiaji na tathmini za utoaji huduma za afya.

Mganga Mkuu wa Mji Dkt. Halima Mangiri (kulia) akiteta jambo na Afisa Ustawi wa Jamii Bi. Jackline Goodluck wakati wa uzinduzi wa Bodi na Kamati ya usimamizi wa huduma za afya.

Bodi itawajibika kwa Halmashauri ya Mji, Jamii (kusimamia utoaji wa huduma bora za Afya) na Wajumbe wote watawajibika kwa waliowachagua. Mjumbe atakayekosa kuhudhuria vikao 3 mfululizo atakuwa amepoteza nafasi ya ujumbe. Kwa wajumbe wote wanaoingia kwa nyadhifa zao watawajibishwa kwa mwajiri kwa kuchukuliwa hatua za kiutumishi. Vile vile Bodi ya huduma za afya itakuwa na uhusiano wa kiutendaji na kamati za usimamizi za vituo. Bodi na kamati ya hospitali zitapokea na kujadili mipango ya Afya ya Halmashauri, pia itasimamia utekelezaji na taarifa ya fedha za kila robo mwaka na kuhakikisha upatikanaji na matumizi ya dawa vituoni.

Katika kutekeleza majukumu yao, Bodi na kamati ya Hospitali zitakutana mara 4 kwa mwaka au zaidi pale inapobidi. Bodi haitaingilia masuala ya kiutaalam ya watumishi ili mradi wapo katika mipaka ya maadili ya kikazi. Kamati ya usimamizi ya Hospitali itawajibika kwa Halmashauri kupitia kwa Bodi ya Afya ya Halmashauri na Jamii katika kusimamia utoaji wa huduma bora za afya Hospitali.


Mwisho.

Picha zote na Nyeneu, P. R

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Timu ya Menejimenti Halmashauri ya Mji Babati imefanya Ziara kukagua Miradi ya Maendeleo

    May 07, 2025
  • Watumishi Manyara wametakiwa kupendana na kuacha chuki.

    April 30, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe.Emmanuela Kaganda amewataka Wananchi kuuenzi Muungano.

    April 26, 2025
  • Chanjo nyongeza ya polio (IPV2) kuanza kutolewa kwa watoto wa miezi 9 mwezi wa tano 2025.

    April 24, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati