• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

BABATI MJI YAVUTIWA NA TANGA JIJI

Imechapishwa: May 19th, 2018


Madiwani na baadhi ya wataalamu  wa Halmashauri ya Mji wa Babati mnamo tarehe 17 na 18 mwezi wa tano walitembelea Halmashauri za Jiji la Tanga na Mji wa Korogwe kujifunza jinsi gani Halmashauri hizo zimeweza kutekeleza miradi yake ya maendeleo.

Katika Halmashauri ya Jiji la Tanga Waheshimiwa Madiwani na Wataalam walitembelea katika stendi  kuu ya Mabasi iliyopo Kange, Duka la dawa za Binadamu lililopo barabara ya nne linalomilikiwa na Halmashauri ya Jiji na Kituo cha runinga cha Tanga Television ambacho pia kinamilikiwa na Halmashauri ya jiji la Tanga.

Akiwakaribisha katika Jiji la Tanga Naibu Meya wa Jiji hilo Bw.Mohamed Haniu  aliwaambia wadiwani na wataalamu wa Halmashauri ya Mji wa Babati siri kubwa ya Mafanikio katika Halmashauri yao ni kuondoa tofauti zao  za kisiasa na kuwatumikia wananchi wa Tanga.”Katika Halmashauri yetu tupo madiwani wa CUF na CCM lakini ukituona tunavyofanya kazi kwa pamoja huwezi kujua diwani yupi wa CUF na yupi ni wa CCM kwani tumekubaliana kuwa Tanga kwanza vyama baadaye” alisisitiza Mheshimiwa Naibu Meya.

Akimshukuru Naibu Meya wa Jiji la Tanga Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Babati Mh.Kibiki M.Kibiki alisema kuwa wamejifunza mengi sana katika Jiji la Tanga na watayafanyia kazi yote waliyoyapata hasahasa suala la kushirikiana bila kujali vyama walivyotoka katika kuwatumikia wananchi wa Babati.

Kuhusu stendi ya Mabasi Madiwani na wataalam wameona jinsi stendi hiyo ilivyokuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa Halmashauri na kuahidi kuanza ujenzi wa stendi Mpya iliyopo eneo la Maisaka Katani haraka iwezekanavyo.

Katika Duka la Dawa za binadamu Madiwani hao waliona jinsi duka hilo linavyoweza kuwahudumia wananchi kupitia zahanati zilizopo pembezoni mwa Jiji la Tanga.

Pia walitembelea kituo cha Television cha Tanga TV kinachondeshwa na Halmshauri hiyo na kuambiwa kituo hicho pia ni chanzo cha mapato kwani kinafanya matangazo ya biashara na kurusha vipindi vya kitaalam mbalimbali kama kilimo, uvuvi, biashara n.k.

Siku  ya pili ya ziara hiyo ambayo ilikuwa  tarehe 18/05/2018 Waheshimiwa Madiwani walitembelea Soko kuu la Kilole na Stendi ya Mabasi ya Kilole iliyopo Halmashauri ya Mji wa Korogwe na kujionea jinsi vyanzo hivyo vya mapato vinavyoweza kuchangia maendeleo ya Mji wetu kama vikisimamiwa kwa umakini.

Akihitisha juu ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Babati ameahidi kuisimamia Halmashauri na kushauri madiwani wenzake kushirikiana juu ya suala la kuleta maendeleo katika Halmashauri ya Mji Babati ili kuacha alama kwa vizazi vijavyo.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Muendelezo wa Ziara ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati Kata kwa Kata katika Halmashauri.

    June 23, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Babati imetembelewa na Maafisa kutoka Skuli ya Bububu Zanzibar

    June 23, 2025
  • Mafunzo yametolewa kwa wanufaika wa mikopo Awamu ya Tatu katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Babati.

    June 21, 2025
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati amefanya ziara katika Kata ya Bonga.

    June 20, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati