• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Babati Mji waadhimisha siku ya afya ya Kinywa na Meno Duniani Mashuleni

Imechapishwa: March 17th, 2021

Na Nyeneu P. R

Katika kuadhimisha siku ya afya ya Kinywa na Meno Duniani, Mratibu wa afya ya kinywa na Meno mkoa wa Manyara Dkt. Pastory Mahendeka ameungana na wataalamu kutoka kitengo cha Meno Halmashauri ya Mji wa Babati pamoja na wataalamu mbalimbali wa afya kutoka Hospitali ya Mji wa Babati, leo tarehe 17 Machi 2021 wameendelea  kutoa elimu mbalimbali na ushauri kuhusu afya ya kinywa na meno mashuleni, ambapo kampeni hiyo ilianza tarehe 15 mwezi Machi 2021 ikiwalenga zaidi wanafunzi wa shule za Msingi.

Daktari Mahendeka ameeleza kuwa, kila mwaka ifikapo mwezi Machi kunakuwa na wiki ya maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa na meno ambapo maadhimisho haya yanakuwa yameambatana na utoaji wa Elimu, Ushauri, Uchunguzi na Matibabu ya Kinywa na Meno.

“Sasa katika hii wiki huwa tunafanya mambo mbalimbali ambayo yanapromote afya ya kinywa na meno. Kwa kawaida huwa tunafanya uchunguzi wa afya ya kinywa na meno kwa makundi mbalimbali hasa Wanafunzi, lakini pia huwa tunafanya matibabu kwa wale ambao watakutwa na matatizo, pia huwa tunatoa Elimu ya afya”. Alisema Dkt Mahendeka.

Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nakwa wakiwa wamekusanyika ili kupata Elimu ya Afya ya Kinywa na meno


Maadhimisho haya yakiwa yamebeba ujumbe “Jivunie Kinywa Chako” Kitaifa yatafanyika mkoani Iringa kuanzia tarehe 15 hadi 20 Machi, 2021 ambapo wananchi wa Iringa na Mikoa jirani watapatiwa Elimu, Ushauri, Uchunguzi na Matibabu ya Kinywa na Meno katika Vituo vya Afya Ngome, Ipogolo na Hospitali ya Frelimo, Huduma ya Upasuaji na Urekebishaji Midomo wazi Itatolewa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.

Wataalam wetu wameendelea kutoa Elimu katika Shule mbalimbali za mji wa Babati ambapo leo tarehe 17 Mwezi Machi 2021 wametembelea Shule ya Msingi Nakwa iliyopo Kata ya Bagara Kijiji cha Nakwa. Kwa kutumia njia shirikishi ya ufundishaji, Wanafunzi wameelimishwa kuhusu aina za meno, kazi za Meno, Magonjwa ya Meno, namna ya kulinda meno, pia jinsi ya kusafisha meno.

Dkt Catherine Mganga kutoka kitengo cha meno Hospitali ya mji wa Babati baada ya somo la namna ya kusafisha meno na kinywa akifuatilia kwa makini zoezi alilompa mwanafunzi kueleza kwa Wanafunzi wenzake namna ya kupiga mswaki au kusafisha kinywa.


Wanafunzi hao wamejifunza pia kuwa kazi mojawapo ya meno ni kukadiria Umri, idadi ya meno yanatumika kutambua umri wa mtoto husika.

“Lakini wakati mwingine pia unakuwa hujui huyu mtoto alizaliwa lini, tunaweza kuangalia kinywani tukakadiria huyu ana miaka 16 au 17, huyu ana miaka Zaidi ya 18. Kwahiyo tunaweza kuangalia kinywani na tukakadiria umri wako”. Alieleza Daktari.

Daktari Mahendeka alisistiza Zaidi wanafunzi kulinda meno yao kwa kupunguza kula vyakula vyenye Sukari, kupiga mswaki (Kusafisha meno) angalau mara mbili kwa siku, kufanya uchunguzi wa meno kila baada ya miezi sita au mwaka mmoja. Elimu hiyo iliambatana na utoaji wa zawadi mbalimbali ikiwemo miswaki, dawa ya meno kwa wanafunzi walioweza kujibu maswali yaliyoulizwa na wataalam hao kwa ufasaha zaidi.

Sambamba na elimu hiyo ya kinywa na meno, pia wataalam wa Afya wametoa Elimu kuhusu Ugonjwa wa Korona (Covid-19) kwa wanafunzi, ambapo wanafunzi wamejifunza Zaidi maana ya Korona, namna Korona inavyoambikzwa, Dalili zake na namna ya kujikinga na Ugonjwa huo. Pia elimu ya macho kutoka kwa mtaalam wa macho Hospitali ya Mji wa Babati ilitolewa kwa wanafunzi hao kwani jicho ni moja kati kiungo muhimu sana katika Maisha ya Binadamu, pia miongoni mwa njia za kupata ugonjwa wa Korona ni Kugusa jicho (macho) na mikono iliyobeba vimelea hivyo.

Mtaalam wa Afya akiwa anauliza maswali mbalimbali yahusuyo ugonjwa wa Korona (Covid -19) kwa wanafunzi na kupewa majibu


Picha zote na Nyeneu, P. R

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Muendelezo wa Ziara ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati Kata kwa Kata katika Halmashauri.

    June 23, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Babati imetembelewa na Maafisa kutoka Skuli ya Bububu Zanzibar

    June 23, 2025
  • Mafunzo yametolewa kwa wanufaika wa mikopo Awamu ya Tatu katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Babati.

    June 21, 2025
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati amefanya ziara katika Kata ya Bonga.

    June 20, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati