• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Vyeti vya Kuzaliwa Bure, lengo ni kuwafikia Watoto zaidi ya 16,000 wenye umri chini ya miaka mitano

Imechapishwa: May 17th, 2021

Na Nyeneu, P. R

Halmashauri ya Mji wa Babati kupitia Hospitali ya Mji, leo tarehe 17 Mei 2021 imefanya uzinduzi wa mpango wa usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano. Katika mpango huo, Halmashauri imejipanga kusajili na kutoa vyeti kwa watoto wapatao elfu kumi na sita mia Saba sitini na nne (16,764) ikiwa ni bila malipo. Aidha Katibu Tawala Wilaya ya Babati Ndg. Halfani Matipula akiwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo akimwakilisha Mkuu wa Wilaya Mhe. Lazaro Twange, ameishukuru sana Serikali kupitia RITA kwa kuleta mpango huo wa vyeti bure katika katika Mkao wa Manyara na wilaya zake zote. 

"Kipekee niishukuru Serikali kwa kuupokea mpango huu na kupitia RITA kuona kwamba kati ya mikao ambayo watapeleka programu hii ni pamoja na Mkoa wetu wa Manyara na kipekee kwa Wilaya yetu ya Babati kwa Halmashauri zote mbili". Alisema DAS.

Uzinduzi wa mpango huu umekuwa ni mwendelezo ambapo wiki iliyopita ulifanyika Halmashauri ya Wilaya ulifanyika katika Kijiji cha Magugu. Ndg. Matipula ameeleza kuwa ili kufikia malengo tuliyojiwekea katika uandikishaji ni lazima taarifa zipelekwe kwa watu wote huko majumbani, hii ni kwa sababu watoto ambao wanapaswa kunufaika na huu mpango si wale tu ambao wazazi wao washiriki katika zoezi la uzinduzi. 

Watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano wanapaswa kuandikishwa na kupatiwa vyeti, na akina mama wasiogope kuwaandikisha watoto wao bila kujali idadi ya watoto alionao.

Sambamba na hayo, pia DAS amesisitiza uadilifu kwa wale watoa huduma wawe mstari wa mbele kuwaambia wananchi kuwa cheti kinatolewa bila malipo yaani bure. Kwani kufanya kinyime na mpango hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yule ambaye atakiuka utaratibu huo wa uandikishaji na utoaji wa cheti bure.

 "Nawaomba sana wale ambao wamepewa majukumu haya wasije hata mara moja wakashawishika kuwaambia wananchi kwamba au kuchukua fedha kwaajili ya kutoa cheti". Amesisitiza Mgeni rasmi. Vile vile Mhe. Mgeni rasmi amewaonya wazazi kutokuthubutu kuwasajili watoto amba sio rai wa Tanzania na wala wasihusike katika kutoa taarifa zao kwa sababu mipango hii ni ya Tanzania na ni kwaajili ya watanzania. 

Aidha, Afya Afya Halmashauri ya Mji Bw. Aretas Leurent akimwakilisha Mganga Mkuu wa Mji katika Hotuba yake ameeleza malengo yao kama Halmashauri katika kuhakikisha zoezi la uandikishaji na utoaji wa vyeti linafikia malengo na pia ameeleza faida za cheti cha kuzaliwa kwa mtu mmoja mmoja. 

  • Kwanza, cheti cha kuzaliwa hutumika kuandikisha watoto wanaoanza elimu ya msingi pia kwa wale wanaoanza elimu ya sekondari. 
  • Pili, cheti kinatumika katika kujiunga na Masomo Elimu ya Juu pamoja na uombaji wa mikopo kupitia Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya juu. 
  • Tatu, Cheti cha Kuzaliwa ni Kitambulisho cha Msingi cha kupata nyaraka nyingine mfano Hati ya Kusafiria pamoja na leseni ya udereva.

Aidha, Afisa Kutoka RITA Mkoa wa Manyara na ni Mratibu Msaidizi wa Zoezi hili la uandikishaji na utoaji wa vyeti bure kwa watoto chini ya miaka mitano Ndg. Temba ameeleza kuwa vyeti hivyo si bure kwa maana ya kuvifanya vikakosa thamani. Akaendelea kwa kusema kwamba vyeti hivyo vimegharamiwa na Shirika la UNICEF ambapo cheti kimelipiwa sawa na vyeti vingine. 

Gharama iliyotumika kukigharamia cheti hiki ni sawa na gharama ya vyeti vingine. Mpango huu uwe ni fursa kwa Wananchi wa Mkoa wa Manyara hususani Wilaya ya Babati na Halmashauri zake zote. Kabla ya mpango, gharama ya kupata cheti cha kuzaliwa ilikuwa ni kubwa kwa maana ya usafiri na muda ukilinganisha na sasa ambapo mtoto wa miaka chini ya mitano atakipata bure na huduma itamfikia popote pale alipo. 

Bw. Temba ametoa rai kwa wananchi kuvithamini vyeti hivyo vinavyotolewa sasa kama wanavyovithamini vile vingine vinavyotolewa maofisini kwani cheti hicho ni sawa na kile ambacho kinapatikana Ofisi za RITA. Cheti hiki kipewe matunzo sawa na kile cheti ambacho umekilipia, Matumizi ni yake yale yale ambayo yangetumika na cheti kile ambacho ungekichukua ofisi za RITA.

Picha zote: Nyeneu, P. R

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga aridhia Miradi ya Mwenge.

    July 03, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Babati amefanya ziara ya kutembelea miradi ya Mwenge wa Uhuru Halmashauri ya Mji Babati

    July 01, 2025
  • Usafi umeendelea katika Machinjio yaliyopo katika Mtaa wa Maisaka B.

    July 01, 2025
  • Mhe.Emmanuela amekabidhiwa gari katika Viwanja vya Mkuu wa Mkoa wa Manyara.

    June 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati