• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Ujumbe wa Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa Wilaya ya Babati

Imechapishwa: August 30th, 2022

Na Nyeneu, P. R

Mkuu wa Wilaya ya Babati ambaye pia ndo Mwenyekiti wa Kamati ya Sensa ya watu na Makazi Wilayani humo Mhe. Lazaro Jacob John Twange amewapongeza Wananchi wote wa Wilaya ya Babati kwa muitikio mkubwa katika zoezi zima la Sensa, Makarani wa Sensa kwa kupita Kaya kwa Kaya, Waratibu wa Sensa na Watumishi wote ambao kwa pamoja wameweza kulifikisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi kufikia hatua hii nzuri tangu lilipoanza tarehe 23 Agosti 2022.

Vilevile DC Twange amesema baada ya kumaliza zoezi la Sensa ya watu siku ya jana tarehe 29 Agosti 2022, kutakuwa na Siku tatu (03) zingine kwaajili ya kuendelea na zoezi la Sensa ya Majengo kuanzia leo tarehe 30 Agosti 2022 hadi tarehe 01 Septemba 2022.

“Naomba nitoe wito kwa Wananchi wenzangu wote wa Wilaya ya Babati kama tulivyotoa ushirikiano katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi lililofanyika kati ya tarehe 23 hadi tarehe 29 Agosti 2022, tuendelee kutoa ushirikiano kwenye zoezi la Sensa ya Majengo linaloendelea kuanzia leo mpaka tarehe 01 Septemba 2022”. Alisisitiza Mhe. DC

Aidha Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema kuwa kama itathibitika kuwepo mtu ambaye kwa bahati mbaya hakuhesabiwa wakati wa zoezi la kuhesabu watu, anaombwa ajitokeze kutumia fursa hii kutoa taarifa kwenye Ofisi ya Kitongoji au Ofisi ya Kijiji, Ofisi ya Mtaa, Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri husika au atoe taarifa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya aweze kuhesabiwa ili kutimiza haki yake ya kizalendo ya kuhesabiwa.

Sambamba na yote hayo, kwa mtu ambaye atapata changamoto yoyote afanye mawasiliano yafuatayo ili aweze kupata msaada bila shida yoyote. Kama ni mkazi wa Halmashauri ya Mji wa Babati piga simu kwa mratibu wa Sensa namba 0784 768 008 na kama ni mkazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Babati piga simu kwa Mratibu wa Sensa namba 0688 105 591. Kama bado utakuwa hujapata msaada tuma ujumbe kwa Mwenyekiti wa Sensa Wilaya ambayo ni 0772 906 333. Ikumbukwe kuwa zoezi la Sensa linasimamiwa kutoka katika ngazi ya Kitongoji, Kijiji, Mtaa, Kata, Tarafa mpaka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

“Zoezi la Sensa Wilaya ya Babati limefanikiwa vizuri na nawashukuru sana Wananchi wa Wilaya ya Babati, Makarani na Wasimamizi wote wa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi, mpaka hivi ninavyozungumza Wilaya ya Babati hatuna tukio lolote la kupotea kwa kifaa chochote maalumu kwaajili ya zoezi la Sensa na tunaahidi hatutoweza kupoteza kifaa chochote cha Matumizi katika zoezi la Sensa kwa sababu ni vifaa adhimu na tuna wajibu wa kuvilinda”. Alimalizia Mhe. Mkuu wa Wilaya.

Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Timu ya Menejimenti Halmashauri ya Mji Babati imefanya Ziara kukagua Miradi ya Maendeleo

    May 07, 2025
  • Watumishi Manyara wametakiwa kupendana na kuacha chuki.

    April 30, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe.Emmanuela Kaganda amewataka Wananchi kuuenzi Muungano.

    April 26, 2025
  • Chanjo nyongeza ya polio (IPV2) kuanza kutolewa kwa watoto wa miezi 9 mwezi wa tano 2025.

    April 24, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati