• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

BODI NA KAMATI YA USIMAMIZI AFYA ZAZINDULIWA.

Imechapishwa: October 30th, 2017


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Babati Mh.Kibiki M. Kibiki amezindua rasmi bodi ya huduma za afya na kamati ya usimamizi ya Hospitali ya Mji wa Babati (Mrara) siku Jumatatu ya tarehe 30/10/2017 katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Babati.

Kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Halmashauri Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mrara Dkt.Charles Mtabho kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji alitoa maelezo kuwa bodi na kamati hizo zimeundwa kufuatia kuisha muda wake mnamo mwezi Juni 2017, Halmashauri ilitangaza nafasi za vyombo hivyo kwa ajili ya kuvihuisha kwani vyombo hivyo huishwa kila baada ya miaka mitatu kisheria.

Akiwahutubia wajumbe hao Mwenyekiti wa Halmashauri aliwasisitiza wajumbe hao waoneshe kuelewa na kuwa tayari kushiriki katika maendeleo ya sekta ya afya katika Halmashauri yetu kwani wapo kisheria.

Mh. Kibiki alisema kuwa mwaka 1994 Wizara ya Afya ilitengeneza utaratibu wa mabadiliko katika sekta ya afya. Mkakati mkuu katika mabadiliko haya ni kurejesha madaraka ya uendeshaji huduma katika Halmashauri na katika ngazi  ya chini kabisa ya jamii kwa kuanzisha Bodi za Huduma za afya na Kamati za Usimamizi  za vituo vya huduma za afya ambazo zitafanya kazi chini ya Halmashauri za serikali za mitaa.

Bodi ya afya inawajibika kwa Halmashauri na ina kazi zifuatazo:

i.    Kujadili na kurekebisha mipango ya Afya na bajeti na kuiwasilisha kwa Halmashauri kwa ajili ya kuidhinishwa;

ii.    Kupokea, kuchambua na kuidhinisha taarifa za utekelezaji kutoka kwa Timu za Uendeshaji wa Huduma za Afya za Halmashauri;

iii.    Kubuni vyanzo mbalimbali vya mapato na kukusanya rasilimali za kutosha kuendesha huduma za Afya za Halmashauri;

iv.    Kushirikiana na Kamati za Afya za Vituo, washirika  wengine kwa nia ya kuinua kiwango cha Afya na utoaji wa huduma;

v.    Kuratibu na kusimamia shughuli za maendeleo ya Afya katika eneo la mamlaka husika.

vi.    Kuisaidia Timu ya Uendeshaji wa Huduma za Afya ya Halmashauri katika kusimamia rasilimali za Afya

vii.    Kuimarisha miundombinu endelevu na mfumo wa mawasiliano na usambazaji.

viii.    Kuhakikisha kunakuwepo wafanyakazi kulingana na ikama ya Halmashauri.

Kamati ya Usimamizi ya Hospitali itatekeleza majukumu kama hayo kwa ngazi ya Hospitali.

A: Wajumbe wa bodi ya afya

1.    Wilson Abong’o     – Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

2.    Hilda Njidile     - Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

3.    Ulumbi Kitundu    - Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

4.    Monica Mollel    - Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

5.    John Kitale        - Mwakilishi kutoka Taasisi/Asasi za Kijamii (NGOs na FBOs)

6.    Julieth Fransis                - Mwakilishi kutoka watoa huduma za afya binafsi.

7.    Jane Wado        - Mwakilishi kutoka Timu ya Uendeshaji Huduma za Afya ya Mkoa

Wajumbe wengine wanne wataingia kwa nyadhifa zao .

8.    Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii

9.    Mganga Mkuu wa Halmashauri

10.     Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mji wa Babati

11.    Afisa Mipango wa Halmashauri

B: Wajumbe wa kamati ya Usimamizi wa Hospitali

1.    Latifa Ally Juma     – Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

2.    Emmanuel Mathew - Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

3.    Toto Mohamed    - Mwakilishi kutoka ngazi ya jamii

4.    Emmanuel Dohho    - Mwakilishi kutoka kamati za vituo vya afya

5.    Alhaji Ramadhani    - Mwakilishi kutoka kamati za zahanati za serikali

6.    John Mumbray    - Mwakilishi kutoka Taasisi/Asasi za Kijamii (NGOs na FBOs)

7.    Michal Nkya    - Mwakilishi kutoka watoa huduma za afya binafsi.

8.    Edastella Ndowo    - Mwakilishi toka Halmashauri aliyeteuliwa na Mkurugenzi  

Wajumbe wengine watatu wataingia kwa nyadhifa zao

9.    Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mji

10.    Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mji

11.    Mwakilishi toka Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mji (CHMT)







Matangazo

  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • Tangazo kwa waliopimiwa na kurasimishiwa viwanja - Sawe na Nangara December 25, 2022
  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kidato cha Kwanza - 2023 December 14, 2022
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • Timu ya Menejimenti Halmashauri ya Mji Babati imefanya Ziara kukagua Miradi ya Maendeleo

    May 07, 2025
  • Watumishi Manyara wametakiwa kupendana na kuacha chuki.

    April 30, 2025
  • Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe.Emmanuela Kaganda amewataka Wananchi kuuenzi Muungano.

    April 26, 2025
  • Chanjo nyongeza ya polio (IPV2) kuanza kutolewa kwa watoto wa miezi 9 mwezi wa tano 2025.

    April 24, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati