• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Barua pepe kwa wafanyikazi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
Babati Town Council
Babati Town Council

Jamhuri ya Muungani wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Babati

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu
      • Idara ya Mipango na Uratibu
      • Idara ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Idara ya Elimu Sekondari
      • Idara ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Miundombinu, Maendeleo ya Vijijini na Mjini
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Fedha na Uhasibu
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo cha Usafi na Udhibiti wa Taka Ngumu
    • Ofisi ya Mtendaji wa Kata
    • Ofisi ya Mtendaji wa Mtaa/Kijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Biashara
    • Kilimo
  • Huduma zetu
    • Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)
    • Utoaji wa Vibali vya Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Mipango Miji na Mazingira
      • UKIMWI
      • Maadili
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Sheria ndogo ndogo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Vyombo
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Habari

Maagizo ya DC Twange kwa Watumishi wa Umma na Wafanyabiashara kuhusiana na utoaji wa risiti za EFD

Imechapishwa: December 2nd, 2022

Na Nyeneu, P. R

Mkuu wa Wilaya ya Babati Mheshimiwa Lazaro Jacob Twange amewaagiza Maafisa Biashara na Maafisa wote wanaohusika wakasimamie zoezi la Matumizi ya Mashine za EFD katika utoaji wa risiti. DC Twange ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Kodi, ametoa maagizo hayo katika kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ambacho kilifanyika Disemba 2, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Babati. Mhe. Twange amesema pia, Wilaya ya Babati haifanyi vizuri kwenye zoezi la utoaji wa risiti kwa mfanyabiashara na kudai risiti kwa mnunuzi. Hatua na adhabu kali zitachukuliwa kwa mfanyabiashara ambaye hata toa risiti na vilevile kwa mnunuzi ambaye hatadai risiti.

Pia Mhe. DC ameongeza kwa kuwaasa watumishi wa umma kuwa mstari wa mbele katika kudai risiti pale wanaponunua kwani watumishi wa umma ndio wanufaika wa kwanza na fedha zinazotokana na kodi kupitia mishahara. "Na sisi watumishi tunajijua, hatudai risiti sisi watumishi. Kwahiyo mtazamo ukibadilika kuanzia kwa sisi watumishi wa umma tunaolipwa mishahara inayotokana na kodi, tunatakiwa tuwe mstari wa mbele kudai risiti." alisisitiza Mkuu wa Wilaya. Mhe. Mkuu wa Wilaya amesema, kwa mtu yeyote atakayekamatwa kwa kosa la kutokutoa risiti au kutokudai risiti, hatokuwa mgeni wake kwa kuwa utaritibu unajulikana na unatakiwa ufuatwe bila kushurutishwa. "Naomba niseme wazi hapa, atakaye kamatwa na atakaye adhibiwa kwa kosa hili, huyu mimi sio mgeni wangu." Aliendelea kusisitiza Mhe. DC.

Mwisho, DC Twange ametoa rai kwa Wafanyabiashara kuwa watii maagizo haya ili wasiipoteze faida inayopatikana na biashara zao katika kulipia adhabu ambayo pengine imesababishwa na uzembe. "Kwahiyo wafanyabiashara kaeni vizuri, maana adhabu yenu ndo kubwa. Na mimi sioni sababu kwenye faida yako usishangae unatoa milioni tatu, milioni Nne na nusu bila utaratibu. Fedha inapatikana kwa mikakati na faida inayopatikana inatakiwa itumike kukuza mtaji wako au kuwekeza zaidi, sasa ukiwa tayari kuipoteza kwenye adhabu ambayo umeifanya kwa udhembe... sisi hatutakuwa sehemu ya kukusaidia kutatua hiyo changamoto. Pambaneni mtii sheria, toeni risiti pale mnapouza na wananchi wadai risiti wanapotoa hela zao kununua."


Picha zote na Nyeneu, P. R

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya pili 2025. May 08, 2025
  • TERMS OF REFERENCE FOR CONSTRUCTION SUPERVISION CONSUTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN BABATI TOWN UNDER TACTIC PRJECT TIER 2 March 07, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI 2025. May 13, 2025
  • Tazama zaidi

Habari Mpya

  • WASOMI KUTOKA CHUO KIKUU CHA MUHAS DAR ES SALAAM WATEMBELEA HALMASHAURI YA MJI BABATI.

    July 24, 2025
  • Bill 19.9 kujenga Stendi ya kisasa, Barabara za kiwango cha lami nzito za Mji km 4.7 na mitaro km 8.15 Halmashauri ya Mji Babati.

    July 24, 2025
  • Wafugaji Halmashauri ya Mji Babati kunufaika na Ruzuku ya 50% ya Serikali ya chanjo za mifugo.

    July 23, 2025
  • Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Babati CPA. Shaaban Mpendu aagiza wakandarasi kusimamia ubora miradi ya Maendeleo.

    July 22, 2025
  • Tazama zaidi

Video

Makala ya Miradi ya Maendeleo Halmashauri ya Mji wa Babati 2024
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Idara ya Habari - Maelezo
  • Salary Slip Portal
  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Mfumo wa Maombi ya Kazi
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Viunganishi Linganifu

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara
  • Halmashauri ya Mji wa Mbulu
  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
  • Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto
  • Halmashauri ya Wilaya Mbulu

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati

    Nukushi: +255-027-2510095

    Simu: +255-027-2510095

    Barua pepe: td@babatitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati