Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga ameweka jiwe la Msingi katika mradi wa maktaba Shule ya Sekondari Sigino ambapo mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi 92,387,000 na unatarajiwa kuzinduliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu.
Mhe.Queen Sendiga amewataka wanafunzi hao kutumia rasilimali za maktaba vizuri ili ziweze kutumiwa na wanafunzi wengine hasa vitabu vitakavyowekwa ili kuongeza kiwango cha taaluma shuleni. Maktaba hiyo itawasaidia takribani wanafunzi 348 na wadau mbalimbali kupitia maktaba hiyo.
Pia Mkuu wa Mkoa ameongoza zoezi la upandaji miti katika eneo la maktaba hiyo ikiwa ni kuhamasisha utunzaji wa mazingira na amewataka wanafunzi hao kutunza hiyo miti ili kufanya maktaba na shule kupendeza na kuwa na mandhari nzuri wakati wote.
Vilevile Mhe.Queen Sendiga amewapongeza wananchi wa Kijiji cha Daghailoy, Kata ya Sigino kwa michango yao ya hali na mali ili kuweza kufanikisha mradi huo wa maktaba shuleni hapo amewataka kuendelea kuchangia katika miradi mengine itakayoletwa katika kijiji chao kwa maendeleo.
Barabara ya Babati - Singida
Sanduku la Posta: P.O.Box 383 Babati
Nukushi: +255-027-2510095
Simu: +255-027-2510095
Barua pepe: td@babatitc.go.tz
Hatimiliki@2021 Haki zote zimehifadhiwa na Halmashauri ya Mji Babati